Najua nikisema biashara unajua kabisa namaanisha nini.
Maana kwenye makala zilizopita nimekuonyesha tofauti ya kumiliki biashara na kumilikiwa na biashara.
Na pia nikakuonyesha tofauti ya kujiajiri ambao ni mfumo mwingine wa utumwa na kumiliki biashara ambayo ndiyo njia pekee ya kufika kwenye uhuru kamili.
Katika yote hayo nimekuwa nazungumzia sana mfumo wa biashara kujiendesha yenyewe.
Wengi wanaposikia hilo la mfumo wanachoka kabisa na kuona ni kitu kikubwa na kinachoweza kufanywa na watu wenye biashara kubwa tu.
Wengi huona wanahitaji kupata wataalamu wa biashara na waliobobea kabisa (MBA) ndiyo waweze kutengeneza mfumo wa kuendesha biashara.
Wengine huona hawawezi kutengeneza mfumo kwa sababu bado hawajawa na wafanyakazi. Hivyo wanaona wasubiri mpaka watakapoanza kuajiri ndiyo wafanye hivyo.
Lakini hayo siyo kweli, unaweza kutengeneza mfumo wa biashara yako wewe mwenyewe na hata kama uko peke yako na biashara ni ndogo.
Kwa hakika ni unapaswa kutengeneza mfumo wa kuiendesha biashara yako haraka iwezekanavyo la sivyo utajitengenezea gereza lako mwenyewe.
Wakati mzuri wa kujenga mfumo kwenye biashara yako ilikuwa wakati unaianza. Wakati mwingine mzuri ni sasa.
Hapa unakwenda kujifunza hatua tano rahisi za kutengeneza mfumo wa biashara yako na nitakushirikisha njia ya kujifunza hatua hizo kwa vitendo kabisa.
Hatua ya kwanza; orodhesha kila kinachofanyika kwenye biashara.
Kila kitu ambacho kinafanywa kwenye biashara, kiorodheshe.
Usiache hata kitu kimoja.
Hatua ya pili; gawa vitu hivyo kwenye makundi yanayoendana. Vitu vinavyohusiana na mauzo vikae pamoja, vinavyohudiana na masoko vikae pamoja. Kadhalika kwenye manunuzi, fedha na uendeshaji.
Hatua ya tatu; elezea kila kitu kinavyofanyika na kwa nini.
Hapa unapaswa kuelezea kila kinachofanyika kwenye biashara jinsi kinavyofanyika na kwa nini kinafanyika hivyo.
Hapa unaeleza mchakato mzima wa kufanya maamuzi kwenye kila eneo la biashara yako.
Hatua ya nne; andika mchakato wa ufanyaji.
Kwa kila maelezo uliyoandaa kwenye kile kinachofanyika kwenye biashara, andika kuwa mchakato ambao utafuatwa na yeyote aliye kwenye biashara.
Unauandika kuwa mwongozo wa kufanya maamuzi kwenye eneo husika ambao utatumiwa na anayefanyia kazi eneo hilo.
Hatua ya tano; hongera tayari una mfumo.
Sasa kusanya miongozo yote ya kila kinachofanyika kwenye biashara na huo ndiyo mfumo wa kuiendesha biashara yako.
Kila kitu kwenye biashara kinapaswa kufanyika kwa kutumia mwongozo huo.
Kila aliye kwenye biashara anapaswa kuusoma, kuuelewa na kuutumia mwongozo huo.
Lakini pia mwongozo huo siyo msaafu, kadiri unavyofanyiwa kazi na kugundua kuna mapungufu au maeneo ambayo hayakuelezewa vizuri, unapaswa kuendelea kuboreshwa kadiri unavyokwenda.
Mpendwa, umejionea hapo mwenyewe, huhitaji elimu kubwa ndiyo uweze kutengeneza mfumo wa biashara.
Unachohitaji ni kukaa chini na kuandika yale ambayo tayari umeshayafanya na kuyageuza kuwa mwongozo.
Chukua hatua hizo tano sasa na utakuja kushukuru mno baadaye.
Kama nilivyokueleza hapo juu, kuna fursa ya kuweza kujifunza hatua hizo tano na kuzifanya kwa vitendo.
Najua wengi mnaosoma hapa mtasema nitafanya, lakini hamtafanya. Mtaendelea kuendesha biashara zenu kwa mazoea na hilo litakuwa kikwazo kwa ukuaji.
Ipo nafasi ya wewe kuchukua hatua hizi na kukamilisha zoezi hilo ndani ya siku moja, ukarudi kwenye biashara yako ukiwa na mwongozo wa kwenda kufanyia kazi.
Kwa hakika ni unapaswa kutengeneza mfumo wa kuiendesha biashara yako haraka iwezekanavyo la sivyo utajitengenezea gereza lako mwenyewe.
Wakati mzuri wa kujenga mfumo kwenye biashara yako ilikuwa wakati unaianza. Wakati mwingine mzuri ni sasa.
Hapa unakwenda kujifunza hatua tano rahisi za kutengeneza mfumo wa biashara yako na nitakushirikisha njia ya kujifunza hatua hizo kwa vitendo kabisa.
Hatua ya kwanza; orodhesha kila kinachofanyika kwenye biashara.
Kila kitu ambacho kinafanywa kwenye biashara, kiorodheshe.
Usiache hata kitu kimoja.
Hatua ya pili; gawa vitu hivyo kwenye makundi yanayoendana. Vitu vinavyohusiana na mauzo vikae pamoja, vinavyohudiana na masoko vikae pamoja. Kadhalika kwenye manunuzi, fedha na uendeshaji.
Hatua ya tatu; elezea kila kitu kinavyofanyika na kwa nini.
Hapa unapaswa kuelezea kila kinachofanyika kwenye biashara jinsi kinavyofanyika na kwa nini kinafanyika hivyo.
Hapa unaeleza mchakato mzima wa kufanya maamuzi kwenye kila eneo la biashara yako.
Hatua ya nne; andika mchakato wa ufanyaji.
Kwa kila maelezo uliyoandaa kwenye kile kinachofanyika kwenye biashara, andika kuwa mchakato ambao utafuatwa na yeyote aliye kwenye biashara.
Unauandika kuwa mwongozo wa kufanya maamuzi kwenye eneo husika ambao utatumiwa na anayefanyia kazi eneo hilo.
Hatua ya tano; hongera tayari una mfumo.
Sasa kusanya miongozo yote ya kila kinachofanyika kwenye biashara na huo ndiyo mfumo wa kuiendesha biashara yako.
Kila kitu kwenye biashara kinapaswa kufanyika kwa kutumia mwongozo huo.
Kila aliye kwenye biashara anapaswa kuusoma, kuuelewa na kuutumia mwongozo huo.
Lakini pia mwongozo huo siyo msaafu, kadiri unavyofanyiwa kazi na kugundua kuna mapungufu au maeneo ambayo hayakuelezewa vizuri, unapaswa kuendelea kuboreshwa kadiri unavyokwenda.
Mpendwa, umejionea hapo mwenyewe, huhitaji elimu kubwa ndiyo uweze kutengeneza mfumo wa biashara.
Unachohitaji ni kukaa chini na kuandika yale ambayo tayari umeshayafanya na kuyageuza kuwa mwongozo.
Chukua hatua hizo tano sasa na utakuja kushukuru mno baadaye.
Kama nilivyokueleza hapo juu, kuna fursa ya kuweza kujifunza hatua hizo tano na kuzifanya kwa vitendo.
Najua wengi mnaosoma hapa mtasema nitafanya, lakini hamtafanya. Mtaendelea kuendesha biashara zenu kwa mazoea na hilo litakuwa kikwazo kwa ukuaji.
Ipo nafasi ya wewe kuchukua hatua hizi na kukamilisha zoezi hilo ndani ya siku moja, ukarudi kwenye biashara yako ukiwa na mwongozo wa kwenda kufanyia kazi.
0 Comments