NEW

6/recent/ticker-posts

Advertisement

Jinsi ya Kutengeneza Vitafunwa vya Kuuza | Maandazi, Skonzi, Karanga

 


Sehemu ya 4: Utengenezaji wa Vitafunwa

Katika sehemu hii ya mwisho, tunakuletea njia za kutengeneza vitafunwa maarufu vinavyopendwa sana: maandazi, skonzi, karanga za mayai, na tambi. Unaweza kuvitumia nyumbani au kuvigeuza kuwa biashara yenye kipato cha uhakika.


🍩 Maandazi

Mahitaji:

  • Unga wa ngano – 1kg
  • Sukari – ¼ kg
  • Baking powder – kijiko 1 cha chakula
  • Amira – kijiko 1 cha chakula
  • Rangi ya chakula – kijiko 1 cha chai
  • Mafuta ya kukandia na kupikia
  • Chumvi kidogo na vanilla (ukipenda)

Hatua:

  1. Umua amira pembeni kwenye kikombe hadi iumuke
  2. Changanya unga, sukari, baking powder, rangi, chumvi na amira
  3. Kanda hadi unga uwe laini, funika uumuke kwa dakika 20
  4. Gawanya na kata umbo la maandazi
  5. Kaanga kwenye mafuta ya moto wa wastani hadi yawe rangi ya kahawia

🍞 Skonzi

Mahitaji:

  • Ngano – 1kg
  • Amira – kijiko 1 cha chakula
  • Mayai – 2
  • Maziwa – ¼ kikombe
  • Sukari – vijiko 4 vya chai
  • Chumvi kidogo

Hatua:

  1. Umua amira na gonga mayai kwenye bakuli, changanya vizuri
  2. Changanya vitu vyote, weka maziwa kidogo kidogo ukikanda
  3. Kata kama chapati
  4. Paka mafuta kwenye sufuria, weka mabonge, funika uumuke
  5. Pika moto wa chini na wa juu kwa utaratibu hadi ziive

🥜 Karanga za Mayai

Mahitaji:

  • Mayai – 2
  • Sukari – ¼ kg
  • Unga wa ngano – ¼ kg
  • Karanga – 1kg
  • Mafuta ya kupikia

Hatua:

  1. Changanya mayai na sukari hadi iyeyuke, weka chumvi kidogo
  2. Weka karanga ndani, nyunyiza unga wa ngano kidogo hadi zipate mchanganyiko
  3. Kaanga kwenye mafuta ya moto wa wastani hadi ziwe za kahawia

🍝 Tambi

Mahitaji:

  • Unga wa dengu – 1kg
  • Baking powder – kijiko 1 cha chakula
  • Pilau masala – kijiko 1 cha chai
  • Pilipili mbuzi – moja (ukipenda)
  • Chumvi
  • Mafuta, jiko, sufuria, mashine ya tambi

Hatua:

  1. Kanda unga kupata uji mzito
  2. Weka kwenye mashine ya kutolea tambi
  3. Pika tambi kwenye mafuta moto kwa kiasi kinachotosha
  4. Baada ya kuiva, chuja na pakia tayari kwa kuuza

📌 Hitimisho

Asante kwa kufuatilia mfululizo wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vitendo. Thubutu, jaribu, fanya mazoezi hadi ubobezi. Mungu akuzidishie maarifa, kipato na mafanikio!

Hakimiliki ©2025 – Jumanne255. Ruhusa ya kushirikisha ipo, lakini tafadhali usibadilishe chochote bila ruhusa ya mwandishi.

Post a Comment

0 Comments